Numbers 23:18-24

18 aNdipo Balaamu akasema ujumbe wake:

“Balaki, inuka na usikilize,
nisikie mimi, wewe mwana wa Sipori.
19 bMungu si mtu, hata aseme uongo,
wala yeye si mwanadamu, hata ajute.
Je, anasema, kisha asitende?
Je, anaahidi, asitimize?
20Nimepokea agizo kubariki;
amebariki, nami siwezi kubadilisha.

21“Haijaonekana bahati mbaya katika Yakobo,
wala taabu katika Israeli.
Bwana, Mungu wao yu pamoja nao,
nayo sauti kuu ya Mfalme imo katikati yao.
22Mungu aliwatoa kutoka Misri;
wao wana nguvu za nyati.
23Hakuna uchawi dhidi ya Yakobo,
wala hakuna uaguzi dhidi ya Israeli.
Sasa itasemwa kuhusu Yakobo
na Israeli, ‘Tazama yale Mungu aliyotenda!’
24Taifa lainuka kama simba jike;
linajiinua kama simba
ambaye hatulii mpaka amalize kurarua mawindo yake
na kunywa damu ya mawindo yake.”
Copyright information for SwhNEN